Wednesday, December 25, 2013

CHEKI POMBE AINA YA ULANZI ILIVYO "DILI" MKOANI MBEYA KATA YA KALOBE

kama kawida siku ya krismas hufanyika katika kipindi ambacho cha mvua .kikawida kabisa kipindi hicho huwa cha ulanzi katika kata ya KALOBE mkoani mbeya.Ambapo vijana wengi wa mtaa wa jua kali hulewa na kupita kiasi.JAMANI ULEVI NOOOOOOOOOOOOOOMAAAAA.IWE KIJANA WA KALOBE ACHA
hapa ulanzi ukiandaliwa
Miti inayotengeneza pombe aina ya ulanzi ikiwa imestawi
Hapa ulanzi ukipelekwa majini tayari kabisa kuwafikia watumiaji.Ulanzi ni moja ya bidhaa inayotegemewa sana na wananchi wengi wa mikoa ya nyanda za juu kwa ajili ya kuwapatia kipatoKALOBE

Sunday, November 17, 2013

BABY ni neno la Kiingereza lenye maana ya mtoto, tena mara nyingi linatumika kwa mtoto mdogo. Pia lina maana nyingine ya mpenzi. Ni neno maarufu sana siku hizi; hata wazee kabisa, utasikia wanaitana baby! Mbali na hilo, yapo maneno mengine kama sweet, dear, honey na mengine mengi. Maneno yote hayo ya Kiingereza, yana maana zaidi ya moja, lakini kubwa zaidi ni kumaanisha mpenzi, mpendwa (hutumika katika kuonesha mapenzi ya dhati kwa mwingine). Leo nataka kukupa kitu kipya kabisa kichwani mwako. Unahitaji utulivu wa hali ya juu ili kujifunza hili. Ni maneno mazuri sana, ya kipekee lakini kwa upande mwingine ni hatari kwa sababu hukaribisha matatizo ambayo hayakutarajiwa na mtumiaji. HUTUMIKA WAPI HASA? “Dear, naomba uniamshe saa 12:00 asubuhi, kesho nina vikao vingi sana asubuhi,” inaweza kuwa kauli ya mume akimwambia mkewe, ambaye naye anamjibu: “Sawa sweet, usijali.” Kwa hakika ndipo sehemu sahihi zaidi kutumika. Ni maneno yenye mshawasha mkubwa na huonesha penzi la dhati lililopo moyoni mwa mhusika kwenda kwa mpenzi wake. Husisimua na kuongeza ladha ya mapenzi ya kweli. Kumuita mpenzi wako kwa majina ya kimapenzi huongeza zaidi upendo na msisimko wa moyo. Mwenzi hujiona wa kipekee na mapenzi huzidi kukua. Kwa maana hiyo basi, ni sahihi zaidi kwa wapenzi kuitana majina niliyotaja hapo juu na mengine yanayofanana na hayo kwa lugha yoyote ile, ila iwe inatambulika vizuri na anayetamkiwa. ATHARI SASA! Kwa upande mwingine kuna athari za kutumia maneno hayo. Zama hizi, maneno hayo yanaonekana ya kawaida tu. Mtu yeyote anaweza kumuita yeyote mpenzi, honey, baby n.k. Hapo ndipo kwenye tatizo lenyewe. Kwa ujumla wanawake ndiyo wanaongoza zaidi kuitana majina hayo. Wakati mwingine huenda mbali zaidi na kuwaita hata wanaume majina hayo ya kimapenzi. Si rahisi kuona athari zake kwa haraka na moja kwa moja, lakini zipo na wengi zimewasababishia matatizo. Ngoja tuone.. HUPUNGUZA THAMANI Kama nilivyotangulia kusema awali, maneno niliyotaja hapo juu husisimua na kuongeza mapenzi. Kwa kuyatumia vinginevyo, basi kwa kiasi kikubwa huanza kukuathiri na kupunguza thamani ya neno lenyewe. Kama unaweza kumwita mfanyakazi mwenzako dear, mtu wa jinsi sawa na wewe sweet ni wazi hata utakapomuita mpenzi wako au wewe kuitwa na yeye, halitakuwa na nguvu sana ya mapenzi kwa sababu ni neno ulilolizoea kila wakati. HUKARIBISHA USALITI Wakati mwingine unaweza kujikuta umeingia kwenye usaliti bila kutarajia. Veronica, mfanyakazi wa saluni moja ya kiume iliyopo Sinza, Dar alitoa ushuhuda ufuatao: “Mimi naishi na mchumba wangu, tuna mtoto mmoja mwenye miaka mitatu. Nafanya kazi saluni. Tangu nimeanza hii kazi, nimejifunza kutumia maneno matamu ya kumfurahisha mteja na wakati mwingine kumfanya akupe tipu baada ya kumaliza kazi. “Kuna kaka mmoja nilizoeana naye sana. Kama kawaida, huwa namkaribisha kwa kumuita dear au sweet. Wakati nikiendelea kumfanyia scrub, mazungumzo yetu hutawaliwa na dear, sweet, nikajikuta nimezidi kumzoea. “Kwa sababu tulibadilishana namba, mara akaanza kuwa na mazoea ya kunitumia meseji, akija ananipa pesa, anaondoka. Mazoea yakazidi. Nikajikuta nimemzoea na kuna siku ambayo siwezi kuisahau kabisa. “Ni siku niliyomsaliti mchumba wangu...mbaya zaidi na huyo jamaa naye ana mke wake. Niliumia sana, lakini naamini kama nisingekuwa na mazoea ya kumuita majina ya kimapenzi nadhani nisingeingia mtegoni. Moyo wangu unauma sana, najuta kumsaliti mpenzi wangu.” Unaweza usione athari hii moja kwa moja, lakini ndugu zangu chukua jambo hili leo; wanaume wengi wakiitwa kwa majina ya kimapenzi husisimka sana – hujiona wenye bahati na mara hushawishika kuingia mapenzi. Kama mwanamke hatakuwa makini atajikuta ametumbukia. Ya nini yote hayo, wakati unaweza kubadilisha mazoea hayo? ANGALIA TOFAUTI Rafiki zangu, kati ya maneno niliyoyataja, kuna ambayo yanakubalika kutumiwa na wasio na uhusiano lakini wawe na undugu wa damu. Mathalani baba, mama, kaka, dada, shangazi nk. Hakuna tatizo kumuita mtu mpendwa, lakini siyo baby, sweet, mpenzi na mengine yenye maana ya moja kwa moja ya kimapenzi. Umenipata? Akili za kuambiwa, changanya na zako kisha unazifanyia kazi! Chukua kinachokufaa! Hadi wiki ijayo kwa mada nyingine. Wewe ni muhimu sana kwangu. Bye!

Saturday, September 14, 2013

AJALI YA GARI YAUA WATU 13 WENGINE 11 WAJERUHIWA VIBAYA,SHINYANGA...!!!

HABARI ZILIZOUFIKIA MTANDAO HUU HIVI PUNDE ZINASEMA KUWA WATU 13, WAMEFARIKI DUNIA NA 11 WAMEJERUHIWA KATIKA AJALI MBAYA ILIYOTOKEA USIKU WA KUAMKIA LEO KATIKA KIJIJI CHA NGONGWA MKOANI SHINYANGA KWENYE AJALI ILIYOHUSISHA GARI AINA YA HICE LENYE NAMBA ZA USAJIRI T 756 CHX NA GARI LILILOKUWA LIMEHARIBIKA LENYE NAMBA ZA USAJILI T 696 AMS. AKIZUNGUMZA KWA NJIA YA SIMU KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA SHINYANGA, KIHEMA KIHEMA, ALISEMA KUWA MIONGONI MWA WATU WALIOFARIKI DUNIA NI PAMOJA NA DEREVA WA HICE, ILIYOKUWA NA ABIRIA HAO IKITOKEA KAHAMA KUELEKEA USHIROMBO AMBAYE ALIFARIKI PAPO HAPO, HUKU MAJERUHI WAKIPELEKWA KUPATIWA HUDUMA YA KWANA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KAHAMA.

Friday, September 13, 2013

Askali wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania katika mpaka wa Tunduma uliopo kati ya Tanzania na Zambia, wamefanikiwa kuzima machafuko yaliyokuwa yameanza kati ya wasafirishaji wa Tanzania na Zambia. Sakata hilo lilitokea juzi kuanzia majira ya saa 2 asubuhi na kumalizika majira ya saa 9 alasiri ambapo wasafirishaji wa upande wa Tanzania walikuwa wakinyang’anya funguo za magari ya raia wa Zambia waliokuwa wakivuka mpakani hapo kwa kile walichodai kuwa walichoshwa na manyanyaso. Walisema kuwa raia wa Zambia wamekuwa wakiwapiga wasafirishaji kutoka upande wa Tanzania hasa wanaosafirisha kwa kutumia Bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda wanapovuka kwenda eneo la Nakonde kupeleka abiria jambo ambalo walilipeleka polisi mara kadhaa lakini walikuwa wakipuuzwa. Wasafirishaji hao walisema kuwa tabia hiyo ya wasafirishaji wa upande wa Zambia imedumu kwa takribani muda wa miezi miwili sasa hivyo nao waliamua kujichukulia hatua mikononi ili Serikali za pande zote mbili zichukue hatua kudhibiti maonezi wanayotendewa. Baada ya hali hiyo kuwa tete, Askari wa Jeshi la polisi katika kituo cha polisi kilichopo Tunduma waliamua kujitokeza na kuwaomba wasafirishaji hao kutoa kero zao na kile kilichosababisha waanze kujichukulia hatua ili kuwadhibiti raia wa Zambia kutoingia na usafiri wao upande wa Tunduma ambapo wasafirishaji hao walitii ombi hilo. Askari Polisi hao wenye vyeo mbalimbali wakiongozwa na mkuu wa kituo hicho Aly Wendo waliwasihi wasafirishaji hao kuacha kufanya hivyo kwa kile walichodai kuwa malalamiko yao yalikuwa ya Msingi lakini wakawaonya kuwa ni muhimu wakaheshimu sheria za nchi zingine. ‘’Tunawashukuru kwa uelewa wenu na kutoa malalamiko bila kuficha na sisi kwasababu tunajua maana ya ujirani mwema na askari wa upande wa pili wanauelewa mzuri hivyo mimi ninaenda kule upande wa pili kuwaeleza wenzangu kuwa kuna jambo hilo hivyo atakayepigwa kuanzia sasa aje kwangu tunavuka nae na kuwakamata wale watakao husika’’ alisema Wendo. Kwa upande wake Inspector Chaburuma na askari wengine ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja waliwafafanulia wasafirishaji hao kuwa sheria za nchi ya Zambia hazitambui usafiri wa Bodaboda na bajaji hivyo ni muhimu wakaheshimu suala hilo licha ya kuwepo mazoea ya ujirani mwema. Kwa upande wao wasafirishaji hao zaidi ya 100 waliokuwa wametoka eneo la mpaka huo walipokuwa wamezingira na kisha kuelekea katika kituo cha polisi baada ya kuombwa na askari polisi wa Tunduma waliwahakikishia askari hao kuwa wamekubaliana na ushauri huo na hasa kutokana na Mkuu huyo wa kituo kuonesha utu wa kufuatilia upande wa pili ili kumalizwa kwa mgogoro unaoweza ukuathiri uchumi wa watu wanaotegemea mpaka huo. Msafirishaji Hamad Omary alisema kuwa kutokana na kueleweshwa na askari hao msafirishaji yeyote ambaye atakiuka makubaliano hayo wenzake hawatahusika na

Padre amwagiwa Tindikali huko Zanzibar

Padri wa kanisa Katoliki Parokia ya Cheju Zanzibar,Joseph Mwangamba amemwagiwa tindikali na kujeruhiwa usoni na kifuani source..East Africa Radio.

YANGA YAITEKA MBEYA

Kikosi cha timu ya Young Africans kimefanya mazoezi yake ya kwanza mkoani Mbeya katika viwanja vya shule ya sekondari Iyunga jioni ya leo kujiandaa na mchezo wake wa Ligi Kuu ya Vodacom siku ya jumamosi dhidi ya timu ya Mbeya City katika dimba la uwanja wa Sokoine. Msafara mkubwa ulijitokeza kukipokea kikosi cha Yanga jana jioni kuanzia maeneo ya kituo cha mafuta cha TAZAMA na kuongozana na mashabiki, wapenzi na wanachama waliojitokeza kuipokea timu mpaka eneo la soweto ilipofikia. Mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara Young Africans wamefanya mazoezi leo kufuatia jana kuwa safarini kutoka jijini Dar es salaam ambapo timu iliwasili majina ya saa 12:30 na kufikia katika hoteli ya Mbeya Paradise Inn iliyopo maeneo ya soweto jijini Mbeya. Wachezaji wamefanya mazoezi chini ya kocha mkuu Ernie Brandts huku wapenzi washabiki na wanachama wakijoitokeza kwa wingi kukishuhudia kikosi cha watoto wa jangwani ambao wameliteka jiji la Mbeya tangu kufika kwake. Mara baada ya mazoezi ya leo kocha ameseam kikosi chake kipo katika hali nzuri kuelekea kwenye mchezo huo wa jumamosi na anaamin timu yake itapata ushindi na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu msimu huu. Aidha viongozi wa Yanga, benchi la ufundi na wachezaji wamefurahishwa na mapokezi waliyoyapaa kutoka kwa wenyeji Tawi la Yanga mkoani Mbeya ambao wamejitolea muda wao wote kuwa na timu bega kwa bega katika maandaliz ya mchezo huo wa jumamosi. Kesho majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki timu itafanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine tayari kabisa kwa kuikabili timu ya Mbeya City siku ya jumamosi. Last Updated ( Thursday, 12 September 2013 18:52 )

Thursday, September 12, 2013

SHIRIKA la Ndege la Precision Air linatarajia kuzindua safari za kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya kuanzia Ijumaa ijayo. Hatua hiyo inafuatia kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe mkoani Mbeya. Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu ya shirika hilo jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uhusiano, Linda Chiza alisema abiria wa safari hiyo, watahudumiwa na ndege aina ya ATR-72, yenye uwezo wa kubeba abiria 70. Alisema kwa mujibu wa ratiba ya shirika, ndege hiyo itakuwa inaruka mara nne kwa wiki kwenda Mbeya na kwamba safari hizo zitaongezeka kwa kadri njia hiyo itakavyoimarika. “Lengo ni kuwapa abiria wetu unafuu wa kuchagua muda wa kusafiri unaowafaa kulingana na ratiba zao,” alisema Linda. “Tunajivunia kuzindua safari hii mpya kuelekea Mbeya ambayo itatuwezesha sasa kuwapatia huduma abiria kutoka Mbeya na Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Alielezea matumaini ya shirika lake kuwa kwa kupeleka huduma hizo mkoani Mbeya, litakuwa linarahisisha usafiri kwa watalii, wafanyabiashara na watu wengine wanaopenda kutembelea mkoa huo wenye utajiri wa vivutio vya utalii. Vivutio hivyo ni pamoja na Mbuga ya Taifa ya Wanyama ya Ruaha na Katavi na Hifadhi nyingine nyingi za taifa. “Tunatambua pia kuwa Mkoa wa Mbeya ni lango la kibiashara kwa nchi jirani za Zambia na Malawi, hivyo kuufanya kuwa mkoa wa kibiashara,” alisema Linda. Alisema uzinduzi wa safari ya Mbeya unafikisha idadi ya maeneo yanayohudumiwa na shirika hilo hapa nchini, kufikia 18 na kulifanya shirika hilo kuwa shirika la ndege kubwa kuliko yote nchini. Aliwahakikishia wateja wa shirika hilo kuwa kampuni yake itaendelea kutoa huduma za usafiri wa anga za kipekee na za uhakika.

Monday, September 9, 2013

Damu ya Yesu yamnasa Mchawi IJUMAA KUU Mbeya ni kijana Jofrey Japhet. Na, Ezekiel Kamanga, Mbeya. KIJANA Jofrey Japhet(18), mkazi wa Kijiji cha Nanyala wilayani Mbozi mkoani Mbeya amenaswa na kile kilichoelezwa kuwa ni nguvu za Mungu siku ya Ijumaa Kuu jana. Tukio hilo limetokea leo eneo la Nzovwe Jijini Mbeya majira ya saa kumi alfajiri katika viwanja vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) ambapo mkutano wa Injili ulikuwa ukiendelea. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi aliyefika mapema eneo la tukio, kijana huyo alisema kuwa alikuwa pamoja na mjomba wake aliyemtaja kwa jina la Edwin Mwakaswila ambaye alimtuma kijana huyo kumchukua binti ambaye alitakiwa waongozane kwenye safari kuelekea Sumbawanga mkoani Rukwa. ��Nilikuwa na Mjomba wangu anayeitwa Edwin Mwakaswila tukielekea Sumbawanga kwa ajili ya kwenda kuongezewa cheo cha nguvu za giza(uchawi) ndipo tulipofika hapa akaniambia niingie kanisani kumchukua Ester Mwashilindi ili tuende nae ndipo nikazidiwa na kushindwa kuondoka ndani ya kanisa walipokuwa wamelala waumini wengi�� alisema kijana huyo. Aidha aliweka wazi kuwa baada ya kuingia ndani ya kanisa hilo kwa ajili ya kumchukua Ester akakosea njia na kumwamusha Enock Mwandagane ambaye alishituka na kumkuta akiwa utupu hali ambayo ikamaliza nguvu za kichawi alizokuwa nazo. Baada ya hapo Mwandagane aliwaamusha waumini wenzake na kuanza kumfanyia maombi kijana huyo huku baadhi ya wasamaria waiwemo wanawake wakimsitiri kwa Kanga utupu wake. Kijana huyo alimtaja Mlafwaya Mwanguluma ambaye anaishi ziwa Rukwa kuwa ndiye mkuu wao wa mambo ya giza ambako ndiko walitarajia kwenda kuongezewa vyeo hivyo vya kichawi ili kijana huyo awe mkuu wa washirikina katika makaburi Jijini Mbeya. Kwa upande wake kiongozi wa huduma ya Maisha mapya ndani ya Kristo (New Life Crist) Amon Mwangosi alisema kijana huyo amekutwa mara nyingi katika mikutano mbalimbali ya Injili akikusudia kuvuruga huduma hiyo ya Mungu hivyo alichukua maamuzi ya kumpeleka katika kituo kidogo cha Polisi cha Nzovwe ili kumwepusha na gadhabu za wananchi wenye hasira kali. Kijana huyo baada ya kufikishwa katika kituo hicho cha polisi aliondolewa na kupelekwa katika kituo kikuu cha polisi kwa gari yenye namba za usajiri T502 AGD.

(CN) - On the 50th anniversary of Martin Luther King Jr.'s "I Have a Dream" speech, his estate sued a nonprofit run by the iconic leader's daughter, claiming she plans to keep using her father's "irreplaceable" memorabilia despite no longer being licensed to do so. In a lawsuit filed Aug. 28 in Fulton County Court, the Estate of Martin Luther King Jr. Inc. -- run by King's sons, Martin Luther King III and Dexter King -- claims it licensed the civil rights activist's intellectual property rights to The Martin Luther King Jr. Center for Nonviolent Social Change in March 2009. The King Center's CEO is Bernice King, the youngest child of the Rev. Dr. Martin Luther King Jr., who was assassinated in 1968. Dr. King's estate claims it supports the center's mission to maintain King's legacy and has been the nonprofit's single largest individual donor for the past decade. But it says the center has been careless with Dr. King's intellectual property, which includes the leader's "name, image, recorded voice and memorabilia," along with "all works of authorship ... including writings, speeches, sermons, letters and copyrights," trademark interests, and "the remains and coffin contained within the crypt of Dr. Martin Luther King Jr." The estate says it conducted an audit in April, which "revealed that the current manner of care and storage of the physical property by defendant is unacceptable." It claims the items are "susceptible to damage by fire, water, mold, and mildew, as well as theft." King's sons say they tried to work with their sister to fix the problems, but the relationship "has recently become strained, resulting in a total breakdown in communication and transparency." As a result, the estate allegedly was forced to terminate the worldwide, royalty- free licensing agreement by mailing the King Center a 30-day notice on Aug. 10. The notice stated that the King Center could prevent its license from being terminated if it agreed to place Bernice on administrative leave pending the final outcome of an audit; get the estate's approval for all responsibilities related to the "use, care and treatment" of the memorabilia; and immediately remove Andrew Young and Dr. King's niece, Alveda King, from its board of directors. The estate claims Alveda tried to "impede" the audit. Bernice, through her personal attorney, responded with a letter indicating that the center "is taking action to work a violation of plaintiff's intellectual property rights," according to the estate. It wants a court order forcing the King Center to stop using its intellectual property after the license expires in September. The estate is represented by William Hill of Rafuse Hill & Hodges in Atlanta. Home Back to Top Courthouse News

picture