Friday, September 13, 2013
Askali wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania katika
mpaka wa Tunduma uliopo kati ya Tanzania na
Zambia, wamefanikiwa kuzima machafuko
yaliyokuwa yameanza kati ya wasafirishaji wa
Tanzania na Zambia.
Sakata hilo lilitokea juzi kuanzia majira ya saa
2 asubuhi na kumalizika majira ya saa 9 alasiri
ambapo wasafirishaji wa upande wa Tanzania
walikuwa wakinyang’anya funguo za magari ya
raia wa Zambia waliokuwa wakivuka mpakani
hapo kwa kile walichodai kuwa walichoshwa na
manyanyaso.
Walisema kuwa raia wa Zambia wamekuwa
wakiwapiga wasafirishaji kutoka upande wa
Tanzania hasa wanaosafirisha kwa kutumia
Bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda
wanapovuka kwenda eneo la Nakonde kupeleka
abiria jambo ambalo walilipeleka polisi mara
kadhaa lakini walikuwa wakipuuzwa.
Wasafirishaji hao walisema kuwa tabia hiyo ya
wasafirishaji wa upande wa Zambia imedumu
kwa takribani muda wa miezi miwili sasa hivyo
nao waliamua kujichukulia hatua mikononi ili
Serikali za pande zote mbili zichukue hatua
kudhibiti maonezi wanayotendewa.
Baada ya hali hiyo kuwa tete, Askari wa Jeshi la
polisi katika kituo cha polisi kilichopo Tunduma
waliamua kujitokeza na kuwaomba wasafirishaji
hao kutoa kero zao na kile kilichosababisha
waanze kujichukulia hatua ili kuwadhibiti raia
wa Zambia kutoingia na usafiri wao upande wa
Tunduma ambapo wasafirishaji hao walitii ombi
hilo.
Askari Polisi hao wenye vyeo mbalimbali
wakiongozwa na mkuu wa kituo hicho Aly
Wendo waliwasihi wasafirishaji hao kuacha
kufanya hivyo kwa kile walichodai kuwa
malalamiko yao yalikuwa ya Msingi lakini
wakawaonya kuwa ni muhimu wakaheshimu
sheria za nchi zingine.
‘’Tunawashukuru kwa uelewa wenu na kutoa
malalamiko bila kuficha na sisi kwasababu
tunajua maana ya ujirani mwema na askari wa
upande wa pili wanauelewa mzuri hivyo mimi
ninaenda kule upande wa pili kuwaeleza
wenzangu kuwa kuna jambo hilo hivyo
atakayepigwa kuanzia sasa aje kwangu tunavuka
nae na kuwakamata wale watakao husika’’
alisema Wendo.
Kwa upande wake Inspector Chaburuma na
askari wengine ambao majina yao hayakuweza
kupatikana mara moja waliwafafanulia
wasafirishaji hao kuwa sheria za nchi ya
Zambia hazitambui usafiri wa Bodaboda na
bajaji hivyo ni muhimu wakaheshimu suala hilo
licha ya kuwepo mazoea ya ujirani mwema.
Kwa upande wao wasafirishaji hao zaidi ya 100
waliokuwa wametoka eneo la mpaka huo
walipokuwa wamezingira na kisha kuelekea
katika kituo cha polisi baada ya kuombwa na
askari polisi wa Tunduma waliwahakikishia
askari hao kuwa wamekubaliana na ushauri huo
na hasa kutokana na Mkuu huyo wa kituo
kuonesha utu wa kufuatilia upande wa pili ili
kumalizwa kwa mgogoro unaoweza ukuathiri
uchumi wa watu wanaotegemea mpaka huo.
Msafirishaji Hamad Omary alisema kuwa
kutokana na kueleweshwa na askari hao
msafirishaji yeyote ambaye atakiuka
makubaliano hayo wenzake hawatahusika na
Padre amwagiwa Tindikali huko Zanzibar
Padri wa kanisa
Katoliki Parokia ya Cheju
Zanzibar,Joseph Mwangamba
amemwagiwa tindikali na kujeruhiwa
usoni na kifuani
source..East Africa Radio.
YANGA YAITEKA MBEYA
Kikosi cha timu ya Young Africans kimefanya mazoezi yake ya kwanza mkoani Mbeya katika viwanja vya shule ya sekondari Iyunga jioni ya leo kujiandaa na mchezo wake wa Ligi Kuu ya Vodacom siku ya jumamosi dhidi ya timu ya Mbeya City katika dimba la uwanja wa Sokoine.
Msafara mkubwa ulijitokeza kukipokea kikosi cha Yanga jana jioni kuanzia maeneo ya kituo cha mafuta cha TAZAMA na kuongozana na mashabiki, wapenzi na wanachama waliojitokeza kuipokea timu mpaka eneo la soweto ilipofikia.
Mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara Young Africans wamefanya mazoezi leo kufuatia jana kuwa safarini kutoka jijini Dar es salaam ambapo timu iliwasili majina ya saa 12:30 na kufikia katika hoteli ya Mbeya Paradise Inn iliyopo maeneo ya soweto jijini Mbeya.
Wachezaji wamefanya mazoezi chini ya kocha mkuu Ernie Brandts huku wapenzi washabiki na wanachama wakijoitokeza kwa wingi kukishuhudia kikosi cha watoto wa jangwani ambao wameliteka jiji la Mbeya tangu kufika kwake.
Mara baada ya mazoezi ya leo kocha ameseam kikosi chake kipo katika hali nzuri kuelekea kwenye mchezo huo wa jumamosi na anaamin timu yake itapata ushindi na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu msimu huu.
Aidha viongozi wa Yanga, benchi la ufundi na wachezaji wamefurahishwa na mapokezi waliyoyapaa kutoka kwa wenyeji Tawi la Yanga mkoani Mbeya ambao wamejitolea muda wao wote kuwa na timu bega kwa bega katika maandaliz ya mchezo huo wa jumamosi.
Kesho majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki timu itafanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine tayari kabisa kwa kuikabili timu ya Mbeya City siku ya jumamosi.
Last Updated ( Thursday, 12 September 2013 18:52 )
Subscribe to:
Posts (Atom)