Monday, September 9, 2013

Damu ya Yesu yamnasa Mchawi IJUMAA KUU Mbeya ni kijana Jofrey Japhet. Na, Ezekiel Kamanga, Mbeya. KIJANA Jofrey Japhet(18), mkazi wa Kijiji cha Nanyala wilayani Mbozi mkoani Mbeya amenaswa na kile kilichoelezwa kuwa ni nguvu za Mungu siku ya Ijumaa Kuu jana. Tukio hilo limetokea leo eneo la Nzovwe Jijini Mbeya majira ya saa kumi alfajiri katika viwanja vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT) ambapo mkutano wa Injili ulikuwa ukiendelea. Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi aliyefika mapema eneo la tukio, kijana huyo alisema kuwa alikuwa pamoja na mjomba wake aliyemtaja kwa jina la Edwin Mwakaswila ambaye alimtuma kijana huyo kumchukua binti ambaye alitakiwa waongozane kwenye safari kuelekea Sumbawanga mkoani Rukwa. ��Nilikuwa na Mjomba wangu anayeitwa Edwin Mwakaswila tukielekea Sumbawanga kwa ajili ya kwenda kuongezewa cheo cha nguvu za giza(uchawi) ndipo tulipofika hapa akaniambia niingie kanisani kumchukua Ester Mwashilindi ili tuende nae ndipo nikazidiwa na kushindwa kuondoka ndani ya kanisa walipokuwa wamelala waumini wengi�� alisema kijana huyo. Aidha aliweka wazi kuwa baada ya kuingia ndani ya kanisa hilo kwa ajili ya kumchukua Ester akakosea njia na kumwamusha Enock Mwandagane ambaye alishituka na kumkuta akiwa utupu hali ambayo ikamaliza nguvu za kichawi alizokuwa nazo. Baada ya hapo Mwandagane aliwaamusha waumini wenzake na kuanza kumfanyia maombi kijana huyo huku baadhi ya wasamaria waiwemo wanawake wakimsitiri kwa Kanga utupu wake. Kijana huyo alimtaja Mlafwaya Mwanguluma ambaye anaishi ziwa Rukwa kuwa ndiye mkuu wao wa mambo ya giza ambako ndiko walitarajia kwenda kuongezewa vyeo hivyo vya kichawi ili kijana huyo awe mkuu wa washirikina katika makaburi Jijini Mbeya. Kwa upande wake kiongozi wa huduma ya Maisha mapya ndani ya Kristo (New Life Crist) Amon Mwangosi alisema kijana huyo amekutwa mara nyingi katika mikutano mbalimbali ya Injili akikusudia kuvuruga huduma hiyo ya Mungu hivyo alichukua maamuzi ya kumpeleka katika kituo kidogo cha Polisi cha Nzovwe ili kumwepusha na gadhabu za wananchi wenye hasira kali. Kijana huyo baada ya kufikishwa katika kituo hicho cha polisi aliondolewa na kupelekwa katika kituo kikuu cha polisi kwa gari yenye namba za usajiri T502 AGD.

No comments:

Post a Comment

picture